"yaah nimesaini mkataba na nitaondoka kwenda kwenye tour hiyo mwanzoni
mwa mwezi wa tisa, imekuwa hivyo kwasababu tunasubiri mwezi mtukufu
upite si unajua tena, kampuni niliyosaini nayo inaitwa DMK global
promotion ambayo ni ya mtanzania ambae anaishi marekani." amesema Dimpoz
nilipomuuliza kuhu mkwanja alioingiza kwa mkataba huo, Dimpoz aligoma kutaja kiasi na kusema
"aaaah unajua tena kwa matatizo yaliyotokea nikitaja tena na mkwanja nilioingiza si ndio itakuwa matatizo kabisa? .
kweli ni uongo wiki iliyopita, kuhusu
kutoa maneno ya dharau kwa Marehem Albert Mangweha a.k.a Ngwea, (ujinga
wake umemfanya afe maskini), Ommy Dimpoz ametokea kupokea makopo na
chupa akiwa stajini (Kili tour) siku ya jumamosi ndani ya dodoma, Ommy
alionekana steji akiwa anaimba na kukwepa makopo kwa wakati mmoja na
baada ya kushindwa kuyavumilia aliamua kuachia stage na kushuka chini na
mwisho kuondoka na kurudi hotelini alipofikia"ndio hivyo, nilikua nimepanda stajini, unajua kutokana na hili
lililotokea, kwa hiyo tangia mwanzo hata mimi wenyewe nilijua labda
kunaweza kukatokea fujo, lakini nilivyopanda watu walinipokea kuliko
nilivyotarajai, kwasababu ndio tumetoka katika vugu vugu hili la,
matatizo haya ambayo yamejitokeza sasa hivi.
kwahiyo ilivyofikia nimemaliza kuimba baadae, unajua hata kama kuna mtu
alipanga kufanya fujo lakini ilikua sasa nguvu hata akipiga yeye akitaka
kutumia nguvu ya watu wanaoshangilia ni wengi, ilipofika wakati naimba
wa me and you, namalizia mwisho ndio kuna baadhi ya mashabiki wakarusha
makopostajini, lakini si unajua mimi mwenyewe nimepitia kumfuu kidogo
kwahiyo nikayapangua, nilicheza nayo paaaaa paaaaaa.
imeenezwa chuki kwamba mimi nimemtukana marehem Albert kitu ambacho sio
kweli, nimejaribu kukielezea kwenye media mbali mbali kuwa si kweli,
wametumia kauli yangu niliyoongea kupitia Killi siku ya Tanzania Music
Awards wakati kitu nilichokiongea nitofauti na kitu kilichokuja
kupandikizwa, lakini mi najua safari ya mziki ni ndefu, na mwenyezi
mungu atajaalia tu haya mambo yatakwisha kwasababu hata yeye mwenyewe
anajua sina kosa, sija mkosea mtu wala sina tatizo na mtu, nafanya tu
maisha yangu ya mziki, lakini inapofikia time unajua mtu mwingine
anaweza akaja tu na sababu zake binafsi kwa nia ya kukuvuta shati,
lakini kama mungu amendika njia yako nyeupe basi itakuwa nyeupe tu, na
hakuna njia iliyonyooka siku zote lazima inakua na vikwazo kidogo, kwa
hiyo naamini hii ni mitihani tu itaisha kwasababu sina tatizo na mtu.
nachoamini binaadam tunakufa pengine roho pengine zinabaki zina hang,
hata marehem mwenyewe naimani anajua kwamba
sikumtukana...................
Msanii kala jeremiah msanii bora wa hip hop aliandika leo kwenye ukurasa wake wa facebook kuwa tuzo alizopata moja anampa marehemu ngwea na kuikabidhi kwa mama yake ngwea alisema
"TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA UMMA KWA UJUMLA
mIMI
KAMA MSANII BORA WA HIP HOP KWA MWAKA HUU NAPENDA KUCHUKUA MUDA HUU
KUWATANGAZIA WATU WOOTE KUWA. KATIKA TUZO TATU NILIZOCHUKUA MOJA
NAIKABIDHI KWA ALBERT MANGWEA.YANI NI TUZO YA MANGWEA NA NITAIPELEKA KWA
MAMA MZAZI WA MANGWEA MOROGORO.
NIMEAMUA
HAYO KWA KUWA HAYATI ALBERT MANGWEA ALIKUWA ANAFANYA MZIKI AMBAO UKO
UPANDE AMBAO MIMI NIMESHINDA TUZO TATU YANI HIP HOP.
TUZO NILIYOAMUA KUMPA MANGWEA NI TUZO YA MSANII BORA WA HIP HOP. KWA KUWA ALIKUWA ANASTAHILI PIA KUITWA HIVYO TUZO
HII NAAMINI ITAKUWA UKUMBUSHO MHIMU SANA KWA FAMILIA YAKE.LAKINI PIA
ITAKUWA INAONYESHA MSHIKAMANO WETU KAMA WASANII WA HIP HOP.''
POPOTE ULIPO KAMA WEWE NI SHABIKI WA HIP HOP TAFUTA NJIA YOYOTE YA KUENDELEA KUMUENZI NDUGU YETU"
Mwanamuziki Naseeb Abduli (diamond) amesema kuwa hashangazwi na mashabiki kumfuata kila anapokatiza kwa kuwa kazi anayofanya siyo ya kitoto.Diamond alipatwa na mkasa wa kuvamiwa na maelfu ya waombolezaji kwenye viwanja vya leaders jijini dar es salaam alipo enda kutoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu Albert Mangwea aliye fariki wiki iliyopita nchini afrika kusini "sishangazwi na hali hiyo bali inaonyesha jinsi gani nafanya kazi nzuri kiasi mashabiki wangu kutaka kuwa karibu yangu muda wote
Mmoja kati ya mshiriki wa mashindano ya kiss nchini china akiwa kwenye pozi huku wakipigana kiss na mpenzi wake mashindano hayo hufanyika kila mwaka nchini humo
kweli duniani kuna vituko haya mashindano ni nouma kweli unaweza kumkiss mpenzi wako kwa muda mrefu bila kupumzika kama unaweza basi unaweza kushiriki kwenye mashindano haya na mshindi hupata yuan 500000 ni sawa na 13milion za kibongo
Staa wa muvi za kibongo "aunt ezekiel mrs demote" amewashtua wadau kwa kuamua kuingia kwenye muziki akizungumza na unstoppble aunt alisema ameamua kujitosa kwenye muziki kwani anaamini yeye ni msanii hivyo anaweza kufanya sanaa ya aina yoyote na alipo kutana na mwanamuziki wa bendi ya mapacha watatu January ndipo walipo pata idea ya kurecod
Tukio hili limetokea maeneo ya mbagala charambe mida ya saa sita mchana
baada ya kibaka huyu kuingia ndani ya nyumba ya mtu na kuiba begi...
Taarifa zinaeleza kwamba, raia mwema ambaye ni mkazi wa nyumba hiyo alisahau kufunga
mlango na kwenda kwa jirani...Alipotoka tu, Kibaka huyo alizama ndani na kuchukua begi la nguo taratiiibu kama
lake!
Hakuridhika na begi, alivyotazama pembeni aliona kuna simu .Bila kupoteza muda, kibaka huyo aliihifadhi
mfukoni ..
Balaa liliazanza wakati anajiandaa kutoka...Alipofika mlangoni, kibaka huyo alikutana na mwenye nyumba uso kwa
uso.....!!!
SINEMA ILIANZIA HAPO!!!!! Watu mwiziii...
mwiziiii mwiziiiiiiiiiii....!!!!!
Kutokana na uzoefu wake wa muda mrefu,
jamaa huyo alibahatika kujisweka ndani jumba bovu lililoko uchochoroni
na kuinusuru roho yake....
Raia
wenye hasira kali hawakumuona wakapita, Kufika mbele kidogo
walikata tamaa. Wakati wanarudi nyumbani kwao mara
ghafla jamaa akakurupuka na kuchomoka kwenye dirisha la lile jengo bovu
alikokuwa amejificha....
Harakati zikaanza upyaaaaaa!!!!! YAAAANI...!! jambazi
hakuchukua raundi akatiwa mikononi...
Mwanadada fatma rashid ndiye nyota wasiku aliyeshiriki kwenye mashindano ya miss bagamoyo yaliyo shirikisha warembo kibao kutoka kila pande za jiji na mwana dada huyo kuibuka namba tano(5) kati ya washiriki saba(7) nakupewa nafasi ya kushiriki miss pwani shindano ambalo lipo karibuni kuanza mwanadada aliku na haya yakusema "kwa sasa nipo najifua ili niweze kushinda kwenye miss pwani sitaki kupata na 3 wala 2 nataka namba moja na asante sana kwa wote walio nipa ushirikiano wa hali na mali nawapenda wote"
kaa tayari kupata track kali kutoka kwake.Msanii huyo alisema "nahitaji support yenu wadau ndo kwanza naingia kwenye game nawahaidi kuwapa vitu vizuri kutoka kwangu nawapenda sana "alisema mwanadada huyo wakati akizungumza na unstoppable ndani ya maisha club.